Imaam an-Nawawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
akakariri [kuomba kuusiwa] ambapo akamwambia tena: "Usighadhibike."
Kauli yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
"Usighadhibike."
Bi maana usijiingize katika njia mbali mbali zinazopelekea katika khasira.
Hivyo, kila njia miongoni mwa njia ambayo inapelekea katika kukasirika, imekatazwa kuindekeza.
Ukiona kitu na wewe unajua fika ndani ya nafsi yako kuwa kitakupelekea katika kukasirika, Hadiyth inaonyesha kuwa ukomeke nacho tokea mwanzo na usikiendekeze na hatimaye ukakasirika na pengine ukashindwa kuzima khasira zako.
Mzungumzaji: Shaykh Swaalih bin ´Abdil-´Aziyz Aalush-Shaykh
Chanzo: Sharh al-Arba´iyn an-Nawawiyyah, uk. 252-253
No comments:
Post a Comment