Thursday, May 12, 2016

JE, NI IPI DAWA YA KHASIRA?

 

عن أبي هُرَيْرَةَ رضي اللهُ عنه أنَّ رَجُلاً قال لِلنَّبِّي صلى الله عليه وسلم: أَوصِني، قالَ:

((لا تَغْضَبْ))، فَرَدَّدَ مِرَاراً، قال: ((لا تَغْضَبْ)).

رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ   

16- Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa kuna mtu alimuomba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amuusie ambapo akamwambia: “Usighadhibike." Yule mtu akakariri [kuomba kuusiwa] ambapo akamwambia tena: "Usighadhibike."

Ni ipi dawa ya khasira? 
Imepokelewa katika Sunnah Hadiyth nyingi kuhusiana na jinsi ya kutibu khasira. Tunazikusanya ifuatavyo:

  1.  Khasira inatibiwa kwa Wudhuu. Mwenye kukasirika ni jambo limewekwa katika Shari´ah akatawadha.
  2.  Akikasirika na hali ya kuwa amesimama anatakiwa kukaa. Huku ni katika kutibu athari za khasira. Kwa kuwa huituliza nafsi yake.
  3. Ajitahidi kujizuia na badala yake alete maneno ambayo ni mazuri. Hili linamuhusu yule anayeweza kufanya hivo.
Mzungumzaji: Shaykh Swaalih bin ´Abdil-´Aziyz Aalush-Shaykh
Chanzo: Sharh al-Arba´iyn an-Nawawiyyah, uk. 254

No comments:

Post a Comment