Thursday, May 12, 2016

JE, INAJUZU KUMPA MWENDAWAZIMU (Kichaa) PESA?

Swali:
Wakati mwingine najiwa na mwendawazimu anayeniomba pesa na anataka kununua chakula. Je, nimpe pesa au naingia katika Kauli Yake (Ta´ala):
وَلَا تُؤْتُوا السُّفَهَاءَ أَمْوَالَكُمُ الَّتِي جَعَلَ اللَّـهُ لَكُمْ قِيَامًا
Wala msiwape wendawazimu mali zenu ambazo Allaah Amekujaalieni kuwa ni msingi wa kujipatia riziki... “ (04:05)
 
Jibu
Mpe walii wake. 
Mwendawazimu lazima awe na walii. Mpe walii wake ili aweze kumhudumia na kumnunulia haja zake. 
Ukimpa mwendawazimu atazichana na hawezi kuzitumia vizuri. Ataziangamiza.

Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

No comments:

Post a Comment