Saturday, April 23, 2016

UZUSHI WAKATI WA KUOMBA DUA



KUFUKIZA UBANI WAKATI WA KUOMBA DUA
بسم الله الرحمن الرحيم
إن الحمد لله، نحمده ونستعينه، ونستغفره، ونعوذ بالله من شرور أنفسنا، وسيئات أعمالنا، من يهده الله فلا مضل له، ومن يضلل فلا هادي له، وأشهد أن لا إله إلا الله وحده لا شريك له وأشهد أن محمدا عبده ورسوله.
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ حَقَّ تُقَاتِهِ وَلَا تَمُوتُنَّ إِلَّا وَأَنتُم مُّسْلِمُونَ ] آل عمران:102   [يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالًا كَثِيرًا وَنِسَاءً ۚ وَاتَّقُوا اللَّهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ ۚ إِنَّ اللَّهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا] النساء:1    [يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ وَقُولُوا قَوْلًا سَدِيدًا ﴿٧٠﴾ يُصْلِحْ لَكُمْ أَعْمَالَكُمْ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ ۗ وَمَن يُطِعِ اللَّهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ فَازَ فَوْزًا عَظِيمًا . الأحزاب:70-71

Sifa zote njema anastahiki Allah aliyetukuka Mola mlezi wa walimwengu wote, swala na salamu zimshukie Kipenzi chetu mtume Muhammad (صلى الله عليه وسلم:) na maswahaba zake mpaka siku ya mwisho.
KUFAA KUTAJA MABAYA  KWA LENGO LA TAHADHARI, NA HASA KTK DINI.

Amesema Imaam Muslimرحمه الله تعالى ktk utangulizi wa: Sahiyh yake:

[وَإِنَّمَا أَلْزَمُوا أَنْفُسَهُمْ الْكَشْفَ عَنْ مَعَايِبِ رُوَاةِ الْحَدِيثِ وَنَاقِلِي الْأَخْبَارِ وَأَفْتَوْا بِذَلِكَ حِينَ سُئِلُوا لِمَا فِيهِ مِنْ عَظِيمِ الْخَطَرِ. إِذْ الْأَخْبَارُ فِي أَمْرِ الدِّينِ إِنَّمَا تَأْتِي بِتَحْلِيلٍ أَوْ تَحْرِيمٍ أَوْ أَمْرٍ أَوْ نَهْيٍ أَوْ تَرْغِيبٍ أَوْ تَرْهِيبٍ فَإِذَا كَانَ الرَّاوِي لَهَا لَيْسَ بِمَعْدِنٍ لِلصِّدْقِ وَالْأَمَانَةِ ثُمَّ أَقْدَمَ عَلَى الرِّوَايَةِ عَنْهُ مَنْ قَدْ عَرَفَهُ وَلَمْ يُبَيِّنْ مَا فِيهِ لِغَيْرِهِ مِمَّنْ جَهِلَ مَعْرِفَتَهُ كَانَ آثِمًا بِفِعْلِهِ ذَلِكَ غَاشًّا لِعَوَام الْمُسْلِمِينَ]

[Na kwa hakika si vinginevyo, Wanachuoni walizilazimisha nafsi zao, kwa kuziweka wazi na kuzifunua aibu za wapokezi wa hadithi na wale wenye kunukuu khabari, na wakatoa fatawa juu ya kufaa kwa hilo pale walipoulizwa. Hilo walilifanya kutokana na kuwa jambo hili la kutowaelezea wapokezi wenye kasoro lina hatari kubwa, kwa sababu khabari zinazohusiana na mambo ya dini huwa zinakuja ima kwa kuhalalisha au kuharamisha, au kuamrisha au kukataza, au kupendezesha jambo fulani, au kutishia jambo hilo. Basi pindi atakapo kuwa mpokezi wa khabari hizo sio mtu wa kujipamba na ukweli na uaminifu, kisha akazitanguliza riwaya au khabari hizo kutoka kwake kwenda kwa yule ambae anamjua, na akawa hakubainisha yale ambayo yapo ktk riwaya hiyo au khabari hiyo –kutokana na udhifu wa khabari hiyokwa yule asiejua khabari hiyo kama ni dhaifu, kufanya kwake hivyo atakuwa amepata madhambi kwa kitendo chake hicho, na atakuwa amewafanyia ghishi wale Waislamu wasio jua]


KWA NINI TUNATOA NASAHA
عن أبي رُقَيَّةَ تَمِيمِ بنِ أوْسٍ الدَّارِيِّ رضي اللهُ عنه: أَنَّ النَّبي صلى الله عليه وسلم قالَ:((الدِّينُ النَّصِيحَةُ)). قُلْنَا: لِمَنْ ؟ قالَ: ((للهِ، ولِكِتَابِهِ، ولِرَسُولِهِ، ولِلأَئِمةِ المُسْلِمِينَ، وعامَّتِهِمْ))
رَوَاهُ مُسْلِمٌ    
Kutoka kwa Abu Ruqayyah Tamim Ibn Aus Addarryرضي الله عنه  ambaye amesema kuwa Bwana Mtume صلى الله عليه وسلم  kasema:
Dini ni nasaha.  Tukauliza: Kwa nani? Akasema kwa Allaah (Kukiri Uungu wake na kwamba Hana mshirika), Kitabu chake (Kukubali kuwa ni maneno ya Allah yasiyo na shaka), na Mtume wake (Kumkubali na kukubali ujumbe aliotumwa nao), na kwa Viongozi wa Waislamu (Kuwatii na kuwafuata katika mema na kuwaasa katika yale wanayokwenda nayo kinyume), na watu wa kawaida (kuusiana mema na kukatazana mabaya kwa njia nzuri).
Imesimuliwa na Muslim

Huu ni ukumbusho ewe ndugu yangu muislamu, na ukumbusho humfaa yule mwenye kuzingatia. Ujumbe huu unahusu Je, kuomba dua kwa kutumia ubani ni katika sunna au ni bid’aa? Majibu ya swali hili ni haya.
Anasema Allah (سبحانه وتعال ) “Na mola wenu anasema: niombeni nitawajibu, kwa hakika wale ambao wanajivuna na kuniabudu mimi wataingia Jahannam wadhalilika” (Ghaafir:60).
Pia kutoka kwa An-Nu’maan bin Bashiyr ( عنها  رضى الله) Mtume  Muhammad (صلى الله عليه وسلم:) amesema  DUA NI IBADA” . (Sunan At-tirmidhy).
Hivyo hakuna anayepinga  swala la kuomba dua ila inatupasa tuombe kwa kufuata njia iliyo sahihi kama tulivyo pata mafunzo Kutoka kwa Mtume Muhammad (صلى الله عليه وسلم:) . Suala la kuomba dua kwa kufukiza ubani katika moto wakati wa kuomba dua ni katika bid’a na haina uhalali , wala faida yoyote na hii imekuwa ni ada kwa ndugu zetu hasa wanaosoma Maulidi na Khitima kwa kuamini kwao kuwa dua’a inapanda juu na moshi wake kama wasemavyo wazushi.
Yote haya ni mambo ya Kijahili(mambo ya kijinga) yasiyokubalika katika sheria ya kiislamu. Allah سبحانه وتعال  anasema “Fuateni mliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wenu” (Al-A’raf :3). Hivyo ni waajib kufuata yale yaliyo teremshwa kutoka kwa Allah na yale aliyotufunza Mtume wetu Muhammad (صلى الله عليه وسلم:) kwa kufuata muongozo ulio sahihi wa mafundisho yake. Pia katika hadiyth sahih Muslim:-  
عن أُمِّ المُؤمِنينَ أُمِّ عَبْدِ الله عائِشَةَ رَضي اللهُ عنها قالَتْ: قالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم: (( مَنْ أَحْدَثَ في أَمْرِنا هذا ما لَيْسَ منهُ فَهُوَ رَد))
 رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ  وَمُسْلِمٌ   وَفِي رِوَايَةٍ لِمُسْلِمٍ
  ((مَن عَمِلَ عَمَلاً لَيْسَ عَلَيْهِ أَمْرُنَا فَهُوَ رَدٌّ )).
Kutoka kwa Mama wa Waislamu  Ummu Abdallah ‘Aisha رضى الله عنها   ambaye alisema:  Mtume wa Allaah سبحانه وتعالى  kasema:
Yule anayezua kitu kisichokuwemo (kisichokuwa) katika jambo (DINI) hili letu kitakataliwa .
Imesimuliwa na Al-Bukhari na Muslim. Na katika usimulizi mwengine wa Muslim inasema hivi:
Yule anayetenda kitendo ambacho hakikubaliani na jambo letu kitakataliwa.
Amesema Abdullah Ibn Mas’uud (رَضي اللهُ عنها).  Fuateni wala msizushe kwa hakika mmetoshelezwa” Hivyo jambo hili la kuomba dua kwa ubani ni katika mambo ambayo hayajafundishwa katika uislamu. Isipokuwa ni uzushi uliozushwana watu , na huku ni kwenda kinyume  na sunna za Mtume Muhammad (صلى الله عليه وسلم:) .
Na kuomba dua kwa kutumia chotezo la moto na ubani hili limechukuliwa kutoka kwa Mafursi (Iran) ambao walikuwa wana abudu “jua na moto.
Mafursi walipoingia katika Uislamu waliingia na baadhi ya desturi zao mbaya zinazokwenda kinyume na uislamu na Mtume Muhammad (صلى الله عليه وسلم:) ametusisitiza sana tusifuate desturi za makafiri na kujifananisha nao.
Mtume Muhammad (صلى الله عليه وسلم:) amesema “Hakika yule atakayeishi katika nyinyi basi atakuja kuona tofauti nyingi , hivyo basi jilazimisheni na sunna zangu na sunna za Makhalifa wangu waongofu wenye kuongoza , ziumeni sunna hizo kwa magego yenu, tahadharini na mambo ya kuzua Hakika kila Bid’aa ni upotofu.”(Sunan Abu-Daud:3607)
Hivyo matendo yote  yanayokwenda kinyume na sunna ni Bid’aa na kwamba kila Bid’aa ni upotovu na kila upotovu ni Motoni. Tuna wauliza wale wenye kuomba dua kwa ubani mafundisho haya wana fundishwa na nani? Kwa sababu  Mtume Muhammad (صلى الله عليه وسلم:) hakulifundisha hili na wala maswahaba hawakulifanya hili.
Na kila kheri basi inapatikana katika karne tatu (3) bora kama alivyo alivyosema Mtume Muhammad (صلى الله عليه وسلم:) na kila shari inapatikana katika mambo ya uzushi, hivyo utaratibu huu si dini bali ni uzushi katika dini ya Allah.
Allah anasema “Enyi mlio amini mtiini Allah na Mtiini Mtume na wenye madaraka katika nyinyi . Mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Allah na Mtume wake mkiwa muna muamini Allah na siku ya mwisho. Hivyo ni njia bora na matokeo mazuri zaidi” (04:59).
Kurejesha kwa Allah ni kurejesha katika Qur’an na kurejesha kwa mtume (صلى الله عليه وسلم:) ni kurejesha katika sunna zake .
Amesema Swahaba Hudheyfah(رَضي اللهُ عنها) Kila ibada ambayo haikufanywa na maswahaba wa Mtume (صلى الله عليه وسلم:) basi usi ifanye ibada hiyo kwa kuwa wale wa mwanzo hawakuacha chochote kwa wamwisho la kuseema,  Mche Allah enyi kongamano la wasomi (Abuu Daud:7064)
Amesema Mtume Muhammad (صلى الله عليه وسلم:) ”Uislamu ulianza ukiwa ngeni na utarejea kuwa mgeni kama ulivyoanza, pongezi kwa wageni” (Muslim:541)  hii ndiyo hali ya sasa kwa wale wanao lingania watu katika usawa, wanaonekana kuwa ni wageni na kutolea hoja zao “mbona jambo hilohilo mimi sikulijua na mbona wazee wetu walikuwa wakilifanya hili
Ewe ndugu yangu muislamu  Mche Allah, TAHADHARI! kisha TAHADHARI! na kila uzushi katika dini na kukaa na watu wa uzushi.
Amesema Allah  (سبحانه وتعال )  “Pindi utakapo waona wale ambao wanafuata mambo yenye utata basi hao ndiyo hao  Allah aliowasema  basi tahadhari nao” (Al-Annisaa:41)
Tunamuomba Allah  (سبحانه وتعال ) aturuzuku kushikamana na Qur’an na Sunna kwa Ufahamu wa wema waliotangulia Mpaka siku tutayo kutana nae.


Imekusanywa na kupangiliwa na
Abu Ayman Sai’d bin Hassan
Tahaqiq
Abuu Khayrat Nadhiru bin Raia

No comments:

Post a Comment