Friday, April 22, 2016

NASAHA KWA WANAWAKE



بِسمِ ٱلله الرَّحْمٰنِ الرَّحِيـمِ.

الحمد لله رب العالمين، والصلاة والسلام على رسول الله خاتم النبيين، وعلى آله وصحبه، ومن والاه إلى يوم الدين.
Ama baada ya kumhimidi Allah na kumtakia sala na salam mtume صلى الله عليه وسلم . Yapaswa utambue kuwa, hakika Allah tabaaraka wata’la aliumba kila kitu katika jinsi mbili na akamuumba mwanadamu katika jinsia hizo [mume na mke] kutokana na tone la manii baada ya kumuumba Adam kwa udongo uliovunda. Hakika zama zimepita na hakuna tofauti katika mwenendo wa Allah tabaaraka wata’la juu ya viumbe wake. Kwani ilipokuwa nafasi ya mwanadamu ni ya juu katika dini kuanzia mwanzo wa ulimwengu mpaka leo, Allah tabaaraka wata’la aliusia utekelezaji wa maamrisho yake kwa wanaadamu na akawausia wanawake pia. Na alikua Mtume صلى الله عليه وسلم akiwausia kwa miongozo hiyo kwenye hotuba katika viwanja vya Arafat
, na sehemu mbalimbali. Kwalo, ni miongoni mwa yanayo ashiria uwajibu wa kutilia umuhimu  kuwakumbusha wanawake katika kila zama, na hasa hasa katika zama hizi ambazo mwanamke wa kiislamu hupigwa vita ili kumporomosh na kumuondosha katika nafasi yake na cheo chake alichopewa na Allah tabaaraka wata’la. Kwa hili, kukawa hakuna budi katika kukumbushana na kutanabahisha khatari inayowakabili wanawake wengi katika zama hizi katika mama zetu na dada zetu na kutaja yale yenye manufaa kwao na sifa ya njia ya mafanikio huenda Allah tabaaraka wata’la kwa tawfiq yake akazifungua nyoyo zilizolala.

KUHUSU MWILI [MAUMBILE] KWA UJUMLA
Fahamu kuwa;
1.      Ni haramu kunyoa au kupunguza nyusi kwa njia yeyote ile ila itakapokuwa hakuna budi kufanya hivyo kwa sababu kunyoa nyusi ni kubadilisha maumbile ya Allah tabaaraka wata’la.
Anasema mtume صلى الله عليه وسلم :

لعن (صل الله عليه و سلم) النامصة والمتنصة

“Amemlaani Mtume (Swallallahu Alayhi Wasallam) ‘an-namiswat’[1] na ‘mutanammiswat”[2]

Na akasema pia صلى الله عليه وسلم :
لعن الله الواشمات و المستوشمات و النامصات و المتنمصات و المتفلجات للحسن المغيرات خلق الله عز و جل

“Allah Amemlaani al-waashimaat na mustawshimaat na an-naamiswaat na al-mutanamiswaat na al-mutafaljaat kwa ajili ya urembo wenyekubadilisha umbile la Allah Mshindi, Mtukufu.”

Na wala haifai kwa mwanamke kumtii mumewe atakapo muamrisha kufanya hivyo , kwa hakika kufany hivyo ni kumuasi Allah tabaaraka wata’la.
Fahamu kuwa;
2.      Na niharamu kwa mwanamke wa kiislamu kunyoa nywele zake zote au kupunguza baadhi yake bila ya dharura ya kisheria na ikiwa anakusudia urembo au kujifananisha na wanawake wa kisasa.
Amesema mtume صلى الله عليه وسلم :

ليس على النساء حلق اِنما على النساء التقصير
Si haki kwa mwanamke kunyoa nywele, hakika hapana vingine isipokuwa ni kupunguza tu[3]
Na wamesema wanachuoni;  kauli yake (Mtume) katika kuzuiwa kunyoa mwanamke kichwa chake “kwani hakika nywele ndefu za wanawake ni kama ndevu kwa wanaume katika muonekano na uzuri . . .[4]
Ama ikiwa kupunguza nywele za kichwa chake ikiwa ni kwa haja isiyokuwa kujipamba kama vile kushindwa kuzitunza au zinarefuka sana na zinampa shida hakuna ubaya katika hili na iwe kwa kiasi cha haja na wala asiziondoe zote. Kama walivyokuwa wake wa Mtume (Swallallahu Alayhi Wasallam) wakifanya baada ya kufa kwake kwa ajili ya kuwacha kujipamba baada ya kufa kwake mtume.[5]
Basi ni juu ya mwanamke kuzihifadhi nywele za kichwa chake na kuziweka mafungu mafungu[6]. Na haifai kwa mwanamke kuzikusanya juu ya kichwa au kuzielekeza kichogoni kama wafanyavyo wengi katika wanawake, bali wengine huweka vibanio ili kujipendezesha na yote haya ni katika mabaya yenye kuchukiza.
Amesema sheikhul-islami ibin tyimiyyahallah amrehemu kuwa “kama walivyokusudia baadhi ya wanawake makahaba kuziweka nywele fungu moja zikiwa ni zenye kupenya baina ya mabega mawili.”[7]
Na amesema sheikh Muhammad bin Ibrahim: “Na ama wanayofanya wanawake wa kiislamu zama zetu hizi katika kuzigawanya pembeni nywele za kichwa na kuzikusanya upande wa kichogoni au kuzijaalia juu ya kichwa kama wanavyofanya wanawake wa kizungu, basi hili halifai kwasababu ya kujifananisha na wanawake makafiri. Kwani;
Amesema Mtume wa Allah صلى الله عليه وسلم :
“namna mbili ni miongoni mwa watu wa motoni sijapatapo waona namna hizo – watu wenye fimbo kama mikia ya ng’ombe wanapiga watu kwa fimbo hizo; na wanawake wenyekuvaa (lakini bado) wapo uchi; wenyekutembea kwa maringo na wanahimiza watu watembee kwa maringo; na vichwa vyao ni kama nundu za ngamia wenye kukonda. Hawatoingia Jannah na wala hawatopata harafu yake, basi hakika harufu yake inapatikana katika masafa kadha wa kadha”[8]

Na hakika wamefasiri baadhi ya wanachuoni kuwa wao wanasuka nywele zao mtindo wa “Maila” nao ni mtindo wa wanawake makahaba.
Na inaruhusiwa kupunguza kwa ibada ya hijjah kiasi cha ‘unmilah’. Akisema Ibn Qudamah (Allah amrehemu):
“Na jambo la sheria kwa mwanamke ni kupunguza kinyume na kunyoa. Hakuna tofauti (ikhtilafu) katika hili”[9]
Fahamu kuwa;

3.      Ni haramu kuziunga au kuzidisha juu yake nywele za mwengine (kuweka rasta au kuzichoma). Nayo ni hukmu ya jumla kwa mwenye kufanyia na mwenye kuwafanyia wenzake kwani;
Amesema mtume صلى الله عليه وسلم :
لعن رسول الله (صل الله عليه و سلم) الواصلة و المستوصلة.
“Amemlaani Mtume wa Allah (Swallallahu Alayhi Wasallam) mwenyekuunganisha na mwenyekuunganishwa”[10]

Na imesimuliwa pia:
Alitoa hotuba wakati alipofika Madina na akatoa kofia la nywele au kifurushi cha nywele kisha akasema: wana nini wake zenu?! , Wanajaalia katika vichwa vyao mfano wa hili? Nimemsikia Mtume (Swallallahu Alayhi Wasallam) anasema “haiwi kwa mwanamke yeyote anaye weka kwenye kichwa chake nywele za mwengine ispokuwa huwa ni udanganyifu (kwa kutumia urembo bandia).”[11]
Fahamu kuwa;
4.      Ni haramu kwa mwanamke wa kiislamu kuachanisha meno yake na kuyachonga kwa tupa mpaka ukatokea kati ya meno yake mwanya mdogo kwa tamaa ya kujiremba.
5.      Ni haramu kwa mwanamke kupaka rangi za kucha ambazo zitazuia maji kufika katika kucha wakati wa kutawadha kama ambavyo haifai kupaka katika sehemu nyingine za mwili kama vile mashavu nk.
Bali kilichosawa kwake ni kupaka HINA kama ilivyonukuliwa kwa mama ‘Aisha allah amuwie radhi:
“hakika mwanamke Fulani alimuliza Aisha (Allah amuwie radhi) kuhusu kupaka hina. Na alisema Aisha: “hakuna ubaya, lakini mimi ninaichukia. Kwa sababu kipenzi changu Mtume wa Allah (Swallallahu Alayhi Wasallam) alikuwa inamchukiza harufu yake.”[12]

Na akasema mtume صلى الله عليه وسلم :

ما أدري أيد رجل أم يد امرأة ؟  قالت : بل يد امرأة : قال : لو كانت امرأة لغيرت أظفارك. – يعني بالحنا 

“sijui ni mkono wa mwanamme au ni wa mwanamke?” alijibu yule mwanamke “bali ni wa mwanamke”: akasema (Swallallahu Alayhi Wasallam) “lau ungelikuwa ni wa mwanmke zingelibadilika kucha zako” akikusudia kwa kupakwa hina.”[13]

6.      Haifai kwa mwanamke (kadhalika mwanaume) kupaka rangi nywele zake, ikiwa ni mvi basi hakika yeye atazipaka kwa rangi isiyo nyeusi kwani, kupaka rangi nyeusi ni jambo lisilofaa.
Kwa sababu ya ujumla wa makatazo yake (صلى الله عليه وسلم) kuhusu kupaka nywele kwa rangi nyeusi. Kama alivyosema Imam An-nawawy katika Riyadhi Swalihina katika mlango wa ‘makatazo ya mwanamke na mwanamme kuhusu kupaka nywele zao kwa rangi nyeusi’.
Ziada:
Yafaa kwa mwanamke kujipamba kutokana na dhahabu na fedha mapambo ambayo yamezoeleka kama bangili na hereni.
Lakini haifai kwa mwanamke kuonyesha mapambo hayo kwa wanaume wanaoweza kumuoa, bali ayafiche hasusan wakati wa kutoka nyumbani na kwenye msongamano wa macho ya wanaume, na ashushe sauti yake mbele yao.

KATIKA MAVAZI
Fahamu kuwa;
1.      Hakika yapasa vazi la mwanamke wa kiislamu liwe zito linalositiri mwili wote ili kuepukana na wanaume wanaoweza kumuoa na hakuna ubaya kupunguza stara kwa wale ambao ni haramu kumuoa na wanawake wenzake. Pia, liwe ni lenye kusitiri ambacho kipo ndani yake, wala lisiwe jepesi (mpaka) inaonekana kutoka ndani yake rangi ya ngozi yake au likabana na likaonesha viungo vyake.
2.      Haifai kujifananisha katika mavazi na wanaume. kwani amelaani Mtume صلى الله عليه وسلم mwanamke mwenye kujifananiza na mwanaume.
3.      Haifai vazi la mwanamke kuwa na mapambo (ambayo yanashawishi) macho (ya watu) kumuelekea wakati wa kutoka nyumbani kwake.
4.      Ni wajibu kwa mwanamke wa kiislam kuvaa juba ambalo litafunika kuanzia kichwani mwake (pamoja na uso wake) mpaka chini.
Kwani imepokelewa kutoka kwa Mama ‘Aisha allah amuwie radhi:

كان الركبان يمرون بنا و نحن مع رسول الله صلى الله عليه و سلم محرمات فاِذا حاذوا بنا سدلت اِحدانا جلبابها من رأسها على وجهها فاِذا جاوزنا كشفناه 
“Walikuwa wapanda farasi wakitupitia na sisi tupo pamoja na Mtume wa Allah (Swalla Allahu Alayhi Wa Sallam) ni wenye kuvaa mavazi ya Ihramu, pindi wanapoelekea kwetu anaachilia mmoja wetu hijabu yake kutoka kichwani kwake juu ya uso wake , na wakitupita tunazifunua”[14]

Na amesema sheikhul-Islamu Ibin Taymiyyah (Allah Amrehemu):
“na hijabu nayo ni vazi lenye kuenea mwilini, nalo ndio ambalo huliita Ibin Mas’ud na mwenzake mtandio na unaweza kuliita ni shuka kubwa. Nayo ni shuka kubwa ambayo hufunika kichwa chake (mwanamke) na sehemu nyengine ya mwili wake. Na hakika alisimulia Abu Ubaidah na mwenzake “hakika yeye (mwanamke) huishusha kutoka juu ya kichwa chake na haonyeshi ispokuwa macho yake na miongoni mwa jinsi yake ni niqabu……”[15]

KATIKA MSIBA
Fahamu kuwa;
1.      Amekataza Allah tabaaraka wata’la kufanya maombolezo katika msiba kwa kunyanyua sauti na kupasua nguo, kujipiga makofi, na kung’oa nywele na kujipaka masinzi usoni na kwa ajili ya kuhuzunika juu ya maiti na dua za majuto na mfano wa hayo yenye kuononesha kuhuzunika kwa ajili ya hukumu ya Allaha na makadirio yake na kukosa subira, kwani;
Amesema mtume صلى الله عليه وسلم  :
 ليس منا من لطم الخدوه و شق الجيوب و دعا بدعوى الجاهلية
Si katika sisi mweny kupiga makofi mashavu yake na kupasua magauni, na kuomba dua za jaahiliyyah (ujinga).
Na akasema pia صلى الله عليه وسلم :

برىء من الصالقة و الحالقة و الشاقة
Amejitenga mwenye    kufanya ‘mwenye kunyanyua sauti yake wakati wa msiba’ na ‘mwenye kunyoa nywele zake wakati wa msiba’ na ‘mwenye kupasua nguo zake wakati wa msiba[16]

Na akasema pia صلى الله عليه وسلم :

لعن النائحة و المستمعة
Amemlaani mwenye kutoa sauti kuomboleza na msikilizaji[17]

NASAHA ZA JUMLA
Fahamu kuwa;
1.      Ni haramu kwa mwanamke kuwapa mikono wanaume wanaoweza kumuoa hata kwa kuweka kitambaa,kanga na mfano wa hivyo katika mkono wake kama wafanyavyo wengi[MAHARIM kwake].
2.      Haifai kuwalaani watoto wadogo na wasiokuwa hao kama wafanyavyo wengi katika wazazi watoto wao wanapokosea.
3.      Ni wajibu [lazima] mwanamke asome dini ya Allah, afanyie kazi, na awafundishe wanawake wenzake na watoto wadogo wa familia yake.
4.      Kwa hakika mwanamke atakaposwali, akafunga, akajihifadhi na akawa mtiifu basi ataingia katika Jannah ya Allah katika mlango autakao. Amesema mtume صلى الله عليه وسلم  :


HITIMISHO

قُلْ لِلْمُؤْمِنِينَ يَغُضُّوا مِنْ أَبْصَارِهِمْ وَيَحْفَظُوا فُرُوجَهُمْ ذَلِكَ أَزْكَى لَهُمْ إِنَّ اللَّهَ خَبِيرٌ بِمَا يَصْنَعُونَ (30) وَقُلْ لِلْمُؤْمِنَاتِ يَغْضُضْنَ مِنْ أَبْصَارِهِنَّ وَيَحْفَظْنَ فُرُوجَهُنَّ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنْهَا وَلْيَضْرِبْنَ بِخُمُرِهِنَّ عَلَى جُيُوبِهِنَّ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا لِبُعُولَتِهِنَّ أَوْ آَبَائِهِنَّ أَوْ آَبَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ أَبْنَائِهِنَّ أَوْ أَبْنَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي أَخَوَاتِهِنَّ أَوْ نِسَائِهِنَّ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُنَّ أَوِ التَّابِعِينَ غَيْرِ أُولِي الْإِرْبَةِ مِنَ الرِّجَالِ أَوِ الطِّفْلِ الَّذِينَ لَمْ يَظْهَرُوا عَلَى عَوْرَاتِ النِّسَاءِ وَلَا يَضْرِبْنَ بِأَرْجُلِهِنَّ لِيُعْلَمَ مَا يُخْفِينَ مِنْ زِينَتِهِنَّ وَتُوبُوا إِلَى اللَّهِ جَمِيعًا أَيُّهَا الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ (31)

30. “Waambie Waumini wanaume wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao. Hili ni takaso bora kwao. Hakika Allah anazo khabari za wanayo yafanya”.
31. “Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao, wala wasioneshe uzuri wao isipo kuwa unao dhihirika. Na waangushe shungi zao juu ya vifua vyao, wala wasioneshe uzuri wao ila kwa waume zao, au baba zao, au baba wa waume zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao, au kaka zao, au wana wa kaka zao, au wana wa dada zao, au wanawake wenzao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume [waliowalea], au wanaume wasio na matamanio, au watoto ambao hawajajua mambo yaliyo khusu uke. Wala wasipige chini miguu yao ili yajuulikane mapambo waliyo yaficha. Na tubuni nyote kwa Allah, enyi Waumini, ili mpate kufanikiwa”[18]

Hizi ni dondoo zilizofupi nasaha [maalum] kwa MAMA,NDUGU ZANGU WA KIKE na [jumla] kwa mwengine atakayesoma risala hii. Namuomba ALLAH anisamehe nilipokosea na anilipe kwa lile nililopatia na atuafikishe mimi na mama yangu na watu wote katika kheri yake. Hakika hakuna mkamilifu isipokuwa Allah.
Makala hii Imeandaliwa na 
ABU KHAYRAT
Nadhiru Ngozi


وصلى الله وسلم على نبينا محمد وعلى آله وصحبه أجمعين


[1] Maana ya an-naamiswat ni mwanamke ambaye hukata nyusi zake.
[2] Maana ya mutanammiswat ni mwanamke mwenye kutata au kukatiwa nyusi.
[3] Abu dawud
[4] Taz: Majmuu’l_fatawa ya sheikh Muhammad Ibrahim 49/2 akinukuu Mirqaat sherh ya Al-mishkaat
[5] Sheikh fawzani katika kitabu chake alichokiita: TANBIHI JUU YA HUKUMU ZA KISHERIA ZINAZOHUSU WAUMINI
   WANAWAKE. na akasema: Na ama ikiwa kusudio la mwanamke katika kuzipunguza nywele zake ni kujifananisha   
   na makafiri wa kike na waovu wa kike au kujifananisha na wanaume basi hilo ni haram bila shaka.
[6] Kuzisuka
[7] Majmuul-fatawa (22/145)
[8] Imam Muslim
[9] Kitabu: Al-mughniy.
   Faida: Amesema Ibin Mundhir; “wamekubaliana maulamaa kwenye jambo hili na hivyo ni kwa
  sababu kunyoa katika haki yao wanawake ni kuchupa mipaka. Kama hivi wamepita Ibn ‘Umar, Imam_shafi’ nk.
[10] Bukhari na Muslim
[11] Bukhari na Muslim
[12] Abu Dawud
[13] An-nasai na Abu Dawud
[14] Abu Dawud, Imam Ahmad na Ibn Majah. (Na hii pia ni dalili ya uvaaji wa niqab kwa mwanamke).
[15] Majmuu’l_fatawa
[16] Bukhari na Muslim
[17] Muslim
[18] Surattn_nuur

No comments:

Post a Comment