بسم الله الرحمن الرحيم
إن الحمد لله، نحمده ونستعينه،
ونستغفره، ونعوذ بالله من شرور أنفسنا، وسيئات أعمالنا، من يهده الله فلا مضل له،
ومن يضلل فلا هادي له، وأشهد أن لا إله إلا الله وحده لا شريك له وأشهد أن محمدا
عبده ورسوله.
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا
اللَّهَ حَقَّ تُقَاتِهِ وَلَا تَمُوتُنَّ إِلَّا وَأَنتُم مُّسْلِمُونَ ] آل عمران:102 [يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا
رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا
وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالًا كَثِيرًا وَنِسَاءً ۚ وَاتَّقُوا اللَّهَ الَّذِي
تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ ۚ إِنَّ
اللَّهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا] النساء:1 [يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا
اتَّقُوا اللَّهَ وَقُولُوا قَوْلًا سَدِيدًا ﴿٧٠﴾ يُصْلِحْ لَكُمْ أَعْمَالَكُمْ
وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ ۗ وَمَن
يُطِعِ اللَّهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ فَازَ فَوْزًا عَظِيمًا . الأحزاب:70-71
أما بعد،
فان أصدق الحديث كتاب الله، وأحسن
الهدي هدي محمد، وشر الأمور محدثاتها، وكل محدثة بدعة وكل بدعة ضلالة، وكل ضلالة
في النار
Hakika ametakasika yule ambaye
amewajibisha na kuamrisha wema na kutimiza haqqi na kuiegemeza kwa kila
anaestahiki na akawajibisha haki kwa wazazi wawili, na ikawa ni amri iliyoenea
kwa walimwengu wote. Hakika ameamrisha ALLAH tabaaraka wata’la katika aya
nyingi kuwafanyia wema na ihsani wazazi wawili.
Mfano wa kauli yake aliposema:
{وَقَضَى
رَبُّكَ أَلاَّ تَعْبُدُواْ إِلاَّ إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً إِمَّا
يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلاَهُمَا فَلاَ تَقُل لَّهُمَا
أُفٍّ وَلاَ تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلاً كَرِيماً* وَاخْفِضْ لَهُمَا
جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي
صَغِيراً}
Na Mola wako Mlezi
ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee
wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie
hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa hishima. Na uwainamishie
bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wangu Mlezi! Warehemu
kama walivyo nilea utotoni.
Akaamrisha
ALLAH tabaaraka wata’la ihsani kwa wazazi wawili katika namna zote za wema, nao
ni katika kauli [unapozungumza nao] pale aliposema [basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa
hishima]. Vivyo hivyo kuwafanyia wema katika matendo; kimwili na kimali kwa
kauli yake aliposema: (Na uwainamishie
bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma).
Na
akanyanyua ubora wanapofika katika hali ya uzee, kisha akakataza kuwavunjia
adabu na kuwatusi, achilia mbali kuwaacha wakiteseka.
UWAJIBU
WA KUWAFANYIA WEMA WAZAZI WAWILI.
Hakika
ameamrisha Allah tabaaraka wata’la, na akawajibisha kwa njia ya wasia
kuwafanyia wema wazazi wawili katika aya nyingi za qur’an. Pale ilipokuja amri
ya wazi juu ya kuwatii, aliposema:
وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ إِحْسَاناً
Na tumemuusia mwanadamu awatendee wema wazazi wake wawili[1]
Ikaonesha
wazi kuwa kuwafanyia wema wazazi wawili ni jambo la wajibu kwa kuwa ni wasia wa
Allah kwetu. Bali akaliambatanisha jambo hilo la kuwafanyia wema wazazi wawili na
twaa’ yake Allah tabaaraka wata’la pale aliposema:
وَقَضَى رَبُّكَ أَلاَّ تَعْبُدُواْ إِلاَّ
إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً
Na mola wako mlezi ameamrisha kuwa msimuabudie
yeyote isipokuwa yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema.[2]
Na kauli
yake aliposema:
وَاعْبُدُواْ اللّهَ وَلاَ تُشْرِكُواْ بِهِ
شَيْئاً وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَاناً
Na mwabudieni Allah wala msimshirikishe na
chochote, na muwafanyie wema wazazi wawili.[3]
Zikakusanya
aya mbili hizi kuwa kufanyiwa wema wazazi wawili ni haqqi yao, bali akaifafanya
haki hiyo kuwa ni ya pili baada ya tawheed yake Allah tabaaraka wata’la
akionesha ukubwa wa jambo hilo [la kuwafanyia wema].
Amesema
Al qurtwubiy [Allah amrehemu], kauli ya Allah “Na wazazi wawili kuwafanyia
wema [ihsani]” maana yake ni:
برهما وحفظهما وصيانتهما وامتثال أوامرهما
Kuwafanyia wema na kuwahifadhi, kuwatunza na kutekeleza amri zao.
Katika
kulisisitiza hilo, mpaka ikawa [wema kwa wazazi wawili] ni wenye kutangulizwa
mbele hata kabla ya Sunnah za kujitolea kama vile Sunnah za kabla ya swala nk.
Na kwa hili akaweka imamu muslim [Allah amrehemu] mlango katika swahih yake
akiuita:
باب تقديم بر الوالدين على التطوع بالصلاة وغيرها
Mlango ambao unaelezea
kutanguliza wema kwa wazazi wawili ni jambo bora kuliko swala za Sunnah na
mengineyo (katika Sunnah za kujitolea)[4]
Kisha
akataja kisa cha Jariyji Ar-raahib[5], akikielezea
abu Hurairah [Allah amridhie] akisema:
وكان
جريج رجلاً عابداً فاتخذ صومعة فكان فيها فأتته أمه وهو يصلي فقالت ياجريج فقال
يارب أمي وصلاتي فأقبل على صلاته فانصرفت فلما كان من الغد أتته وهو يصلي فقالت :
ياجريج , فقال : يارب أمي وصلاتي فاقبل على صلاته , فانصرفت , فلما كان من الغد
أتته وهو يصلي , فقالت : ياجريج , فقال : أي رب أمي وصلاتي فاقبل على صلاته ,
فقالت : اللهم لاتمته حتى ينظر إلى وجوه المومسات ـ يعني الزانيات ـ فتذاكر بنو
إسرائيل جريجاً وعبادته وكانت امرأة بغي يتمثل بحسنها فقالت إن شئتم لأفتننه لكم ,
قال : فتعرضت له فلم يلتفت إليها فأتت راعياً كان يأوي إلى صومعته فأمكنته من
نفسها فوقع عليها فحملت فلما ولدت قالت : هو من جريج , فأتوه فأنزلوه وهدموا
صومعته وجعلوا يضربونه , فقال : ما شأنكم , قالوا : زنيت بهذه البغي فولدت منك ,
فقال : أين الصبي فجاءوا به , فقال : دعوني حتى أصلي فلما انصرف أتى الصبي فطعن في
بطنه , وقال : ياغلام من أبوك ؟ قال : فلان الراعي , فأقبلوا على جريج يقبلونه
ويتمسحون به وقالوا : نبني لك صومعتك من ذهب, قال : لا أعيدوها من طين كما كانت
ففعلوا .
. . . Na alikuwa Juraij mwenye
kufanya ibada nyingi (mwenye taqwa), akajifanyia kijumba akawa (anafanya ibada)
humo. Akamjilia mama yake (mzazi) na hali ya kuwa (Juraij) yu katika swala,
akaita ((kumwita mwanae)): ((Ewe Juraij)), akasema Juraij: ((Ewe mola wangu, mama
yangu [ananiita nikiwa katika] swala yangu)), akaendelea na swala yake,
akaondoka (mama mzazi) na alipofika kesho yake akaja tena na hali yakuw Juraij
yu katika swala, akaita: ((Ewe Juraij)), akasema Juraij: ((Ewe mola wangu, mama
yangu [ananiita nikiwa katika] swala yangu)), akaendelea na swala yake, akasema
(mama): ((Ewe Allah !usimfishe mpaka akutane na uso wa kahaba)). Zilienea
khabari za Juraij na ibada zake kwa banu israeel. Na kulikuwa na mwanamke
kahaba ambaye ni mzuri wa kiwiliwili akasema (kuwaambia watu): mkitaka nitamtia
fitna (nitamhadaa Juraij na kumtia kwenye uovu): akajipeleka kwa Juraij, na
Juraij hakumjali, akamwendea mchungaji ambaye alikuwa akiishi karibu na nyumba
ya Juraij na akafanya naye uovu na akapata ujauzito, zama alipozaa akasema
(yule mwanamke kuwaambia watu): huyu ni mtoto wa Juraij, watu wakamjia (Juraij)
wakamtoa ndani, wakaivunja nyumba yake na wakaanza kumpiga. Akasema (Juraij):
((ni lipi jambo lenu?)) wakasema: ((umezini na kahaba huyu na ukakuzalia
mtoto)) akasema: ((yupo wapi huyo mtoto?)) wakaja naye, akasema: ((niacheni
niswali)) alipomaliza kuswali akamjilia mtoto akamminya tumboni na akamuuliza:
((Ewe kijana, ni nani baba yako?)) akasema (yule mtoto): ((fulani mchungaji)),
wakamuelekea (watu) Juraij wakawa wakimkumbatia, wakimbusu na wakimgusa
(wakikusudia baraka) na wakasema: ((tunajiandaa kukujengea nyumba yako kwa
dhahabu)) akasema: ((hapana, ijengeni kwa mchanga kama mlivyoikuta mwanzo)).[6]
Tazama
jinsi gani twaa’ ya mzazi ilivyokuwa ni jambo la thamani na lenye kheri na
kuwaasi wao ni jambo la shari. Hakika wito wa mzazi ulikuwa bora zaidi kuliko
swala za sunnah alizokuwa akiziswali kwani, mama alipoomba dua akalikubali
Allah dua lake kwa dhati ya mzazi kwa mwanae. Kwani mtume صلى الله عليه وسلم katika hadithi ambayo ameihadithia abuu Hurairah
[Allah amridhie] akisema:
((
ثلاث دعوات لا ترد : دعوة الوالد لولده ،
ودعوة الصائم ، ودعوة المسافر ))
Dua za watu watatu hazirudishwi: dua ya mzazi
kwa mwanae, na dua ya aliyefunga, na dua ya msafiri.[7]
Na katika riwaya nyingine akisema:
(( ثلاث دعوات مستجابات لا شك فيهن ، دعوة الوالد على ولده ، ودعوة
المسافر ، ودعوة المظلوم ))
Dua za watu watatu ni zenye kujibiwa: dua ya
mzazi kwa mwanae, na dua ya msafir, na dua ya aliyedhulumiwa.[8]
Bali yatakiwa kuwapendelea wao na kuwatanguliza katika mambo yote
ya kheri zaidi ya yeyote baada ya Allah na mtume wake,
Na yatosha uwajibu wa mtu kumhudumia mzazi wake kwa yale
aliyoyataja mtume صلى الله عليه وسلم kwani,
سألت رسول الله صلى الله عليه وسلم : أي العمل أحب إلى الله ؟
قال : الصلاة على وقتها ، قلت : ثم أي ؟ قال : بر الوالدين ، قلت : ثم أي ؟ قال :
الجهاد في سبيل الله "
Aliulizwa mtume wa Allah صلى الله عليه وسلم : ni
ipi a’amali inayopendwa Zaidi na Allah ? akasema: swala katika wakati wake, nikasema:
kisha ipi? (Akasema): kuwafanyia wema wazazi wawili, nikasema: kisha ipi?
Akasema: jihaad katika njia ya Allah.[9]
Akajaalia mtume صلى الله عليه وسلم wema kwa wazazi wawili ni bora zaidi
kuliko jihadi katika njia ya Allah, na halikuwa hilo isipokuwa kutokana na
ukubwa na uwajibu wake.
UJUMLA
WA NAMNA ZA WEMA KWA WAZAZI NA MALIPO YAKE
Ndugu katika iyman, tambua kuwa wema kwa wazazi
wawili ni katika njia ya mitume na Akalitaja jambo hilo Allah tabaaraka wata’la
katika aya nyingi ndani ya qur’an. Kwalo akamsifia yahya [‘alayhis_salaam]
akisema:
وَبَرًّا بِوَالِدَيْهِ وَلَمْ يَكُن جَبَّارًا عَصِيًّا
Na akawa mwema kwa wazazi wake, wala hakuwa
Jabari muasi[10]
Na akamsifu pia kwalo jambo hilo ‘Iysa [‘alayhis_salaam] akisema:
وَبَرًّا بِوَالِدَتِي وَلَمْ يَجْعَلْنِي جَبَّارًا شَقِيًّا
Basi ikawa hakuna kufaulu wala kutengenekewa duniani na
akhera isipokuwa kupitia kwao. Na likapata nguvu jambo hili kwa kauliya mtume صلى الله عليه وسلم kutoka kwa ibn ‘Abbas [Allah
amridhie] akisema:
(( من أصبح مطيعاً لله في والديه أصبح له بابان مفتوحان من الجنة
وإن كان واحداً فواحد، ومن أمسى عاصياً لله في والديه أصبح له بابان مفتوحان من
النار، وإن كان واحداً فواحد، قال رجل : وإن ظلماه ؟ قال : (( وإن ظلماه، وإن
ظلماه، وإن ظلماه )) .
Atakaepambaukiwa akiwa katika twaa’ ya Allah kwa wazazi wake
atakuta milango miwili ya Jannah imefunguliwa kwa ajili yake, na ikiwa ni
[mzazi] mmoja basi ni [mlango] mmoja, na atakayefikwa na jioni hali yakuwa
amemuasi Allah kwa wazazi wake atakuta
milango miwili ya motoni imefunguliwa kwa ajili yake, , na ikiwa ni
[mzazi] mmoja basi ni [mlango] mmoja, akasema mtu: hata kama atamdhulumu?
Akasema: ((hata kama atamdhulumu, hata kama atamdhulumu, hata kama atamdhulumu)).
Na likatajwa jambo hilo hata ikawa kuwaasi
wao ni katika madhambi makubwa yenye kuangamiza, kwani anasema mtume صلى الله عليه وسلم katika hadithi
aliyoipokea Abu Bakrata [Allah amridhie]:
(ألا أنبئكم بأكبر
الكبائر؟) ثلاثا قالوا: بلى يا رسول الله قال: (الإشراك بالله وعقوق الوالدين)
وجلس وكان متكئا (ألا وقول الزور) ما زال يكررها حتى قلت ليته سكت
(Je,
nikujulisheni [nikukhabarisheni kuhusu] madhambi makubwa kuliko yote?)
(akayasema maneno haya mara tatu), wakasema (maswahaba): tujuze ewe mtume wa
Allah! Akasema: (kumshirikisha Allah na kuwaasi wazazi wawili) kisha akaketi,
[kanakwamba] ilikuwa somo limeisha, [kisha akasema] ([pia] na kiapo cha uongo)
hakuacha kuwa akilikariri (akilirejerejea) hili mpaka nikajisemea (moyoni)
laity angenyamaza[12]
Ikajulisha kuwa ni jambo lisilofaa kuwaasi
na kuwahama wazazi, bali kumtusi ni jambo la muhali, tena lisilofaa zaidi kama
alivyosema mtume صلى الله عليه وسلم katika
riwaya nyingine akisema:
(( من أكبر الكبائر شتم الرجل والديه قالوا : يا رسول الله وهل
يشتم الرجل والديه قال : (( نعم ، يسب أبا الرجل فيسب أباه ، ويسب أمه فيسب أمه ))
Miongoni
mwa madhambi makubwa ni mtu kumtusi mzazi wake, wakasema (maswahaba): ewe mtume
wa Allah! Na je mtu anamtusi mzazi wake? Akasema: ((ndio, anamtusi mtu baba wa
mwenzie naye anamtusi babaye, na anamtusi mtu mama wa mwenzie naye anamtusi
mamaye))[13]
Bali
mtume صلى الله عليه وسلم akatangaza laana kwa yule mwenye kumlaani mzazi wake, akisema:
(( لعن الله من لعن والديه))
[ صحيح الأدب المفرد ] .
Amemlaani
Allah mwenye kumlaani wazazi wake[14]
Hata ikawa Jannah ni haramu kwa yule mwenye kuwaasi
wazazi wawili pale aliposema mtume صلى الله عليه وسلم :
ثلاثة حرم الله تبارك وتعالى عليهم الجنة، مدمن الخمر، والعاق،
والديوث الذي يقر الخبث في أهله
Watu
wa namna tatu, Allah tabaaraka wata’ala ameharamisha juu yao [kuingia] Jannah,
aliyekubuhu katika ulevi, na mwenye kuwaasi wazazi wawili, na duyuth[15]
ambaye anaridhia uchafu katika familia yake([16])
[17]
Na akasema pia:
كل الذنوب يؤخر الله منها ما شاء إلى يوم القيامة إلا عقوق الوالدين،
فإن الله يعجله لصاحبه في الحياة الدنيا قبل الممات
Madhambi yote huchelewesha Allah kutokana nayo madhambi hayo [kwa
adhabu] vile atakavyo mpaka siku ya kiama isipokuwa kuwaasi wazazi wawili,
hakika ya Allah humharakishia [adhabu] mwenye kuwaasi wazazi wake katika maisha
ya dunia kabla ya mauti [yake][18]
Kwahiyo
Allah tabaaraka wata’la akaweka makemeo makali kuhusiana na kuwafanyia ubaya na
kuwaasi na kuwalaani wazazi wawili katika dalili hizo na zisizokuwa hizo katika
hadithi zenye kutaja makemeo makali kwa mwenye kuwaasi wazazi wawili.
Kama
hivyo ndivyo, basi tambua:
Hakika miongoni mwa wema kwa wazazi ni
kuwalisha, kuwavisha na kuwanywesha, kadhalika kuzungumza nao maneno laini na
kutowafanyia kibri, baba anahangaika usiku na mchana akitafuta cha kukulisha
kama ambavyo mama anahangaika kumnyonyesha mwanae na zaidi ya hayo. Na miongoni
mwa mambo mema ambayo kwayo Allah amewajibisha kuwafanyia wazazi ni kuwahurumia
na kuwaombea dua.
Anasema
Allah tabaaraka wata’la:
وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ
مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيراً
Na uwainamishie bawa la unyenyekevu
kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wangu Mlezi! Warehemu kama walivyo nilea
utotoni.[19]
Tambua
kuwa, kuwafanyia wema wazazi katika namna yoyote iwayo, ni sababu ya mtu kuiingia
Jannah ya Allah tabaaraka wata’la. Hakika amehadithia Abu huraira [Allah
amridhie], kutoka kwa mtume صلى الله عليه وسلم :
رغم أنفه، رغم أنفه، رغم أنفه، قيل: من يا رسول الله؟ قال من أدرك والديه
عند الكبر أحدهما أو كليهما ثم لم يدخل الجنة
Imegota chini pua yake, imegota chini pua yake,
imegota chini pua yake, pakasemwa: ni nani (huyo) ewe mtume wa Allah? Akasema:
aliyewadiriki wazazi wake katika uzee, mmoja wao au wote wawili kisha hakuingia
Jannah.[20]
Ikajulisha kuwa, kuwafanyiawema wazazi au mmoja kati yao ni katika
sababu za mtu kuingia Jannah na kuepushwa na moto.
Na kuwafanyia wema ni katika sababu za kupata nusra ya Allah
tabaaraka wata’la katika mabalaa, kama anavyohadithia mtume صلى الله عليه وسلم kutokana na hadithi ya watu watatu ambao
walifunikwa na jiwe pangoni, pale aliposema mmoja wao:
( اللهم كان
لي أبوان
شيخان كبيران
وكنت لا
أغبق قبلهما
أهلاً ولا
مالا، فنأى
بي طلب
الشجر يوماً
فلم أرح
عليهما حتى
ناما فحلبت
لهما غبوقهما
فوجدتهما نائمين
فكرهت أن
أوقظهما فلبثت
والقدح على
يدي انتظر
استيقاظهما حتى
برق الفجر
فاستيقظا فشربا
غبوقهما ،
اللهم إن
كنت فعلت
ذلك ابتغاء
وجهك ففرج
عنا ما
نحن فيه
من هذه
الصخرة ،
فأنفرجت شيئاً.....)
(Ewe Allah,
nilikuwa mimi nina wazazi walio wazee, na nilikuwa siipi familia yangu maziwa
kabla yao, siku moja, nilichelewa kurudi siku moja kwa bahati mbaya, nikafika
nikiwa nimechelewa nao wakiwa wamekwisha lala, nilikamua maziwa kwa ajili yao
ni nikawakuta wamelala, nikachukia kuwapa maziwa familia yangu kabla ya wao.
Nikawasubiri na bakuli la maziwa li mkononi mwangu mpaka waamke hadi ikanikuta
alfajiri, kisha wakaamka na wakanywa mziwa yao. Ewe allah ikiwa nilifanya kwa
ajili yako basi tupe faraja sisi kutokana na hali tuliyonayo kutokana na jiwe
hili, jiwe likasogea kidogo lakini hawakuweza kutoka)[21]
Kisha ikawa
kuwafanyia wema wazazi wawili ni katika sababu za na kukunjuliwa rizki kwa
ujumla wa kauli yake mtume صلى الله عليه وسلم aliposema:
من أحب أن يبسط له في رزقه وينسأ له في أثره فليصل رحمه
Yule
anaetaka akunjuliwe katika rizki yake na kurefushwa umri wake basin a aunge
undugu[22]
Na katika riwaya nyingine
akasema:
من سره أن يمد له في عمره ويزاد في رزقه فليبر والديه وليصل رحمه
Yule anayetaka kuongezewa katika umri wake na azidishiwe katika
rizki yake basi na amfanyie wema mzazi wake na aunge udugu[23]
Na zikawa radhi za
Allah tabaaraka wata’la zi pamoja na radhi za wazazi kwa kauli ya mtume صلى الله عليه وسلم aliposema:
رضا الرب في رضا الوالد ، وسخط الرب في سخط الوالد
Radhi za Allah zi katika radhi za mzazi, na chuki ya Allah i-
katika chuki ya mzazi[24]
Na katika riwaya
nyingine
رضا الرب في رضا الوالدين و سخطه في
سخطهما
Radhi za Allah zi katika radhi za wazazi wawili, na chuki ya Allah
i- katika chuki yao[25]
Tazama ni ukubwa kiasi
gani Allah tabaaraka wata’la akifadhilisha darja la wazazi mpaka kufikia kuwa
humridhia mja maadamu mja huyo ameridhiwa na wazazi wake katika mipaka ya
kisheria na humghadhibikia na kutokuwa radhi naye yule ambaye ameghadhibikiwa
na wazzazi wake.
Bila ya shaka, hakika wema wa wazazi ni jambo
kubwa na lenye fadhila nyingi hata na wizani wake ni wizani wa juu hata ikawa
kuulipa wema wake huo ni jambo zito, kwani mtume صلى الله عليه وسلم katika hadithi
iliyoihadithia Abu Huraira Allah amridhie amesema:
لا يجزي ولد والداً ، إلا أن يجده مملوكاً فيشتريه فيعتقه
[Kamwe] mtoto haweza lipa wema kwa baba,
isipokuwa atakapomkuta mtumwa, akamnunua akamwacha huru[26]
MIPAKA YA KISHERIA KATIKA KUWATII WAZAZI WAWILI
Hakika pamoja na kutajwa uwajibu wa kuwatii wazazi,
pakatajwa pia kuwa twaa’ hiyo iwe ni katika wema na si uovu. Itakapokuwa amri
ni katika kumuasi Allah tabaaraka wata’ala [iwe ni amri ya kulifanya jambo ovu
au kuacha wajibu] hakika Allah tabaaraka wata’la ameikemea twaa’ hiyo pale
aliposema:
{ وَإِن جَاهَدَاكَ عَلَىٰ أَن تُشْرِكَ بِي مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ
فَلَا تُطِعْهُمَا ۖ وَصَاحِبْهُمَا فِي الدُّنْيَا مَعْرُوفًا ۖ وَاتَّبِعْ
سَبِيلَ مَنْ أَنَابَ إِلَيَّ ۚ ثُمَّ إِلَيَّ مَرْجِعُكُمْ فَأُنَبِّئُكُم بِمَا
كُنتُمْ تَعْمَلُونَ }
Na pindi wakikushikilia kunishirikisha na ambayo huna elimu nayo,
basi usiwatii. Lakini ishi nao kwa wema duniani, nawe ishike/ifuate njia ya
anayeelekea kwangu. Kisha marejeo yenu ni kwangu, name nitakujulisheni
mliyokuwa mkiyatenda[27]
Allah akaamrisha kutowatii pamoja na daraja lao kwa mtoto
wao, na hilo likatajwa kuwa ni miongoni mwa utimilifu wa imani ya mja, akisema:
لا تَجِدُ قَوْمًا يُؤْمِنُونَ
بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الآخِرِ يُوَادُّونَ مَنْ حَادَّ اللَّهَ وَرَسُولَهُ
وَلَوْ كَانُوا آبَاءَهُمْ أَوْ أَبْنَاءَهُمْ أَوْ إِخْوَانَهُمْ أَوْ
عَشِيرَتَهُمْ أُوْلَئِكَ كَتَبَ فِي قُلُوبِهِمُ الإِيمَانَ وَأَيَّدَهُم بِرُوحٍ
مِّنْهُ
Huwakuti
watu wanaomuamini Allah na siku ya mwisho kuwa wanawapenda wanaompinga Allah na
mtume wake, hata wakiwa ni baba zao, au watoto wao, au ndugu zao au jamaa zao.
Hao ameandikakatika nyoyo zao Imani, na akawapa nguvu
kwa roho itokayo kwake[28]
Akasema pia:
يَا أَيّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا
آبَاءَكُمْ وَإِخْوَانكُمْ أَوْلِيَاء إِنْ اِسْتَحَبُّوا الْكُفْر عَلَى
الْإِيمَان وَمَنْ يَتَوَلَّهُمْ مِنْكُمْ فَأُولَئِكَ هُمْ الظَّالِمُونَ
Enyi
mlioamini ! msiwafanye baba zenu na ndugu zenu kuwa vipenzi vyenu ikiwa
wanastahabu [wanapenda] ukafiri kuliko Imani. Na katika ninyi atakayewafanya
kuwa ndio vipenzi vyake, basi ndio madhwaalim[29]
Na
jambo hilo la kutomtii mzazi katika kumuasi Allah tabaaraka wata’la kwasababu yeye
ni kiumbe, na kiumbe hana ukubwa wa kuzidi mipaka ya Allah tabaaraka wata’la:
kama anavyosema mtume صلى الله عليه وسلم :
لا طَاعَةَ لأَحَدٍ فِي مَعْصِيَةِ اللَّهِ ,
إِنَّمَا الطَّاعَةُ فِي الْمَعْرُوفِ
Hakuna
twaa kwa yeyote katika kumuasi Allah, kwa hakika utiifu [kutii] ni katika mema[30]
Akasema pia:
لا طاعةَ لمخلوقٍ في معصية الخالق
Hakuna
twaa kwa kiumbe katika kumuasi muumba[31]
KUJUZU KWANASIHI WAZAZI WANAPOKOSEA
Fahamu
kuwa, Nasaha ni jambo ambalo limefanywa kuwa nguzo ya dini, ni juu ya mtoto
kumnasihi babae kwa wema kama ilivyo juu ya mzazi kumnasihi mwanae
atakapokengeuka katika mafundisho ya dini. Na hili ndio lililokaribu Zaidi na
kufikia katika maisha ya furaha ya dunia na kuipata Jannah ya Allah tabaaraka
wata’la.
Ansema mtume صلى الله عليه وسلم kupitia hadithi ya Tamiym Ad-darimy:
الدين النصيحة ، قلنا : لمن يا رسول الله ؟ قال : لله ، ولكتابه ،
ولرسوله ، ولأئمة المسلمين وعامتهم
dini
ni nasaha, tukasema kwa nani ewe mtume wa Allah? Kwa Allah, na kitabu chake, na
mtume wake, na viongozi wa waislam na watu wote[32]
Fahamu
kuwa nasaha kwa wazazi ndio njia mitume na waja wema waliotangulia katika zama
za nyuma na zama hizi pia.
Anasema Allah tabaaraka wata’la:
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ يَا أَبَتِ لِمَ تَعْبُدُ مَا لَا يَسْمَعُ وَلَا يُبْصِرُ وَلَا يُغْنِي عَنْكَ شَيْئًا (*) يَا أَبَتِ إِنِّي قَدْ جَاءَنِي مِنَ الْعِلْمِ مَا لَمْ يَأْتِكَ فَاتَّبِعْنِي أَهْدِكَ صِرَاطًا سَوِيًّا
Aliposema
[Ibrahim a.s] kumwambia baba yake: Ewe baba yangu! Kwa nini unaviabudu visivyo
sikia, na visivyoona na visivyo kufaa kwa chochote? Ewe baba yangu! Kwa yakini
imenifikia elimu isiyokufikia wewe. Basi nifuate mimi, name nitakuongoza njia
iliyo sawa[33]
Na Allah akaamrisha
kushikamana na mila hii ya Ibrahiim [‘alayhis_salaam] akasema:
وَجَاهِدُوا فِي اللَّهِ حَقَّ جِهَادِهِ هُوَ اجْتَبَاكُمْ وَمَا جَعَلَ عَلَيْكُمْ فِي الدِّينِ مِنْ حَرَجٍ مِّلَّةَ أَبِيكُمْ إِبْرَاهِيمَ
Na
fanyeni juhudi kwa ajili ya Allah ukweli wa kufanya juhudi. Yeye amekuteueni.
Wala hawakuweka juu yenu mambo mazito katika Dini. Nayo ni mila ya baba yenu
Ibrahim[34]
Na zisizokuwa hizo katika aya nyingi zenye kujulisha
hilo. Na ikawa malipo yao kwa nasaha hizo ni Jannah, kama anavyosema Allah
tabaaraka wata’la.
جَنَّاتُ عَدْنٍ يَدْخُلُونَهَا وَمَنْ صَلَحَ مِنْ آبَائِهِمْ وَأَزْوَاجِهِمْ وَذُرِّيَّاتِهِمْ ۖ وَالْمَلَائِكَةُ يَدْخُلُونَ عَلَيْهِمْ مِنْ كُلِّ بَابٍ
Jannah
ya milele, wataiingia wao na walio wema miongoni mwa baba zao, na wake zao, na
vizazi vyao. Na malaika wanawaingilia katika kila mlango[35]
NAFASI YA MAMA KWA BABA NA BABA KWA MAMA KATIKA WEMA
Hakika
sharia ya dini imemtanguliza mama kabla ya baba katika wema na ikawa ni fadhwla
za Allah tabaaraka wata’la kwa mama. Na hili ni kwa sababu ya udhaifu na
unyonge wake katika kukabiliana na mambo. Hakika mama ndie ambae amekubeba
tumboni mwake miezi tisa, akakuzaa kwa shida, akakunyonyesha, akakulea kwa
huruma huku akikesha kwa homa zako na taabu zako, hudhikika yeye kwa dhiki zako
kama ambavyo alikuwa akihangaika ili kuleta faraja yako.
Kwani anasema Allah tabaaraka wata’la:
وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حَمَلَتْهُ أُمُّهُ
وَهْناً عَلَى وَهْنٍ وَفِصَالُهُ فِي عَامَيْنِ أَنِ اشْكُرْ لِي وَلِوَالِدَيْكَ
إِلَيَّ الْمَصِيرُ
Na tumemuusia mtu kwa wazazi
wake wawili, mama yake ameichukua mimba yake kwa udhaifu juu ya udhaifu na
kumwachisha ziwa baada ya miaka miwili (tukamuusia kuwa) nishukuru mimi na
wazazi wako wawili, (na) kwangu ndio marejeo (yenu).[36]
Akasema pia:
وَوَصَّيْنَا الْإِنْسَانَ بِوَالِدَيْهِ إِحْسَانًا ۖ حَمَلَتْهُ أُمُّهُ كُرْهًا وَوَضَعَتْهُ كُرْهًا ۖ وَحَمْلُهُ وَفِصَالُهُ ثَلَاثُونَ شَهْرًا ۚ
Na
tumemuusia mwanadamu awatendee wema wazazi wakewawili. Mama yake amechukua
mimba kwa taabu, na akamzaa kwa taabu. Na kuchukua mimba kwake hata kumwachisha
ziwa ni miezi thelathini[37]
Anasema mtume صلى الله عليه وسلم katika hadithi ambayo ameihadithia Abu Hurairah akisema :
جاء رجل إلى رسول الله
فقال : يارسول الله، من أحق الناس بحسن صحابتي ؟ قال : ((أمك)) قال : ثم من ؟ قال : ((أمك)) قال : ثم من ؟ قال : ((أمك)) قال : ثم من ؟ قال : (( أبوك)).
Alikuja mtu kwa mtume wa Allah akasema: Ewe mtume wa Allah, ni nani
(mtu) mwenye (kustahiki) haki Zaidi kwa wema wa usuhuba (wangu)? Akasema:
((mama yako)), akasema (tena yule mtu): kisha nani? Akasema: mama yako? akasema
(tena yule mtu): kisha nani? Akasema: mama yako? akasema (tena yule mtu): kisha
nani? Akasema: baba yako[38]
Na
katika upokezi mwingine aliulizwa mtume صلى الله عليه وسلم :
يارسول الله من أحق الناس بحسن الصحبة ؟ قال : (( أمك ثم أمك ثم أمك ثم أبوك ثم أدناك أدناك ))
Ewe mtume wa Allah ni nani mwenye haki zaidi miongoni mwa watu kwa
kumfanyia wema wa usuhuba (kusuhubiana)? Akasema (mtume): ((mama yako, mama
yako, mama yako kisha baba yako, kisha wa chini yako))
Ikawa haki ya wema kwa mama ni yenye kunyanyuliwa mara
tatu dhidi ya haki ya baba, na hili ni kutokana na darja alilopewa na Allah
tabaaraka wata’la na kufadhwilishwa kwake dhidi ya baba. Bali inasimuliwa Asmaa
bint Abu bakr Allah amridhie:
قدمت على أمي وهي مشركة في عهد رسول الله ، فاستفتيت رسول الله قلت : قدمت على أمي وهي راغبة ( طامعة عندي تسألني شيئاً ) أفأصل أمي ؟ قال : (( نعم صلي أمك ))
Alikuja kwangu mimi mama yangu katika zama za mtume
s.a.w, na hali yakuwa ni mshirikina, nikamtaka fat_wa mtume wa Allah صلى الله عليه وسلم nikasema kumwambia; amenijia
mimi mama yangu na hali yakuwa akihitajia kutoka kwangu [nimsaidie shida yake]
je, niendeleze uhusiano na mama [kwa kumsaidia shida yake]? Akasema: ndio
endeleza uhusiano na mama yako[39]
Na hakulikubali hilo mtume صلى الله عليه وسلم isipokuwa
kwa ukubwa wa haki ya mzazi [hasa mama] kwa mwanae, isipokuwa ni kwa sababu ya
unyonge na udhaifu wake. Kwani hakuna jambo lililokubwa zaidi kuliko kumtimizia
mama haja yake anapokuwa na shida. hata akasema Ibn ‘Abbas [Allah amridhie]:
(( إني لا أعلم عملاً أقرب إلى الله عز وجل من بر الوالدة )).
Mimi siijui a’amali yenye kumkaribisha (mtendaji) kwa Allah mwenye
‘izza na utukufu kuliko kumfanyia wema mama[40]
Na akalifanya Allah
jambo hilo kuwa ni katika sababu za mtu kusamehewa na kufutiwa madhambi yake. Kwani
Amesimulia Abu bakr ibn Hafswa Allah amridhie kuwa, alikuja mtu kwa mtume صلى الله عليه وسلم akasema:
يارسول الله إني أصبت ذنباً عظيماً ، فهل لي من توبة ؟ قال : هل لك من أم ؟ قال : لا ، قال : هل لك من خالة ؟ قال : نعم ، قال : فبرها ]
Ewe mtume wa Allah ! mimi nimefanya dhambi kubwa, je nina toba
(ninaweza samehewa)? akasema (mtume): je, unaye mama? Akasema: hapana, akasema
(mtume): je unaye shaangazi? Akasema: ndio, akasema (mtume): basi kamfanyiewema[41]
Na katika hadithi ya Al-baraa amesema mtume صلى الله عليه وسلم :
[ الخالة بمنزلة الأم ]
Shangazi yu- katika daraja la mama[42]
Na
kasha akakataza mtume صلى الله عليه وسلم juu ya kumuasi mama akimpwekesha kutokana na baba akisema:
إن الله حرم عليكم عقوق الأمهات
Hakika Allah ameharamisha juu yenu kuwaasi wazazi wa kike
[mama zetu].[43]
Tambua
pia, pamoja na darja kubwa alilopewa mama dhidi ya baba, hakika mtume صلى الله عليه وسلم anasema:
الوالد أوسط أبواب الجنة
Baba ni mlango wa katikati (wa) Jannah([44])
HITIMISHO
Nimalizie kwa kusema; pale nilipopatia basi
ni kwa uwezo wa Allah tabaaraka wata’la na pale nilipokosea basi mapungufu
yanarudi kwangu kwa kuwa ni muhari kujinasibishia ukamilifu kwani ukamilifu ni
wa Allah tabaaraka wata’la.
وصلى الله وسلم على نبينا محمد وعلى آله
وصحبه أجمعين
Imekusanywa
na kuandikwa na
ABU HUDHEYFAH
Tahqiqy
ABU KHAYRAT
Nadhiru Ngozi
[1]
Al-ahqaaf 15
[2]AL-
Israa 23
[3]
An-nisaa 36
[4]
Sahih muslim
[5]
Kupitia yeye mtoto mdogo alizungumza, na ikawa ni mmoja kati ya watoto watatu
ambao walizungumza utotoni.
[6] Bukhari
na muslim
[7]
Sahihul jamii’, (sheikh Albany r.a)
[8]
Sahihul jamii’, (sheikh Albany r.a)
[9]
Bukhari na Muslim
[10]
Maryam 14
[11]
Maryam 32
[12]
Imam Bukhari
[13]
Bukhari na Muslim
[14]
Sahih Muslim
[15]
Duyuth ni mtu ambaye, uchafu unafanyika kwa watu wa nyumbani kwake miongoni mwa
dada zake, wanawe na
mkewe lakini
haongei wala hakemei bali anaona sawa tu
[16]
Na makusudio ni uchafu wa zinaa na mengineyo katika machafu.
[17]
Imam Ahmad
[18]
At-twabarany (Al_kabeer), Al-haakim (Al_awsatw), Imam Bukhari (Aadabul_mufrad)
[19]Al-
Israa 24
[20]
Bukhari na Muslim
[21]
Bukhari na Muslim
[22]
Bukhari na Muslim, imesimuliwa na Anas ibn Maalik.
[23]
Bukhari na Muslim
[24]
At-tirmidhy, silsilatus-swahih.
[25]
At-twabarany
[26]
Muslim
[27]
Suratul_luqmaan 15.
[28]
Suratul_mujaadillh 22
[29]
Suratut_tawbah 23
[30]
Bukhari na Muslim
[31]
Imam Ahmad
[32]
Bukhari na Muslim
[33]
Surat Maryam 42-43
[34]
Suratul hajj 78
[35]
Suratur_raad 23
[36]
Luqmaan 14
[37]
Suratul Ah’qaaf 15
[38]
Bukhari na Muslim
[39]
Bukhari na Muslim
[40]
Imam Bukhari [Aadabul_mufrad]
[41]
Albaghwiy katika shirh sunnah
[42]
Bukhari na Muslim
[43]
Bukhari na Muslim, amehadithia hadithi hii ‘iysa al mughiyra Allah amridhie
[44]
At-tirmidhy na Ibn Majah
No comments:
Post a Comment