Wednesday, May 11, 2016

UTOFAUTI KATI YA SHAKA NA WASIWASI

Swali:  
Ni shaka ipi ambayo ni kufuru? 
Je, shaka ya khiyari juu ya kuwepo kwa Allaah (Ta´ala) au ukweli wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)…

Jibu: 
 Kuna tofauti ya wasiwasi na shaka. Shaka haijuzu
Pamoja na hivyo wasiwasi unaweza kumjia mtu na akapambana nao kwa kumuomba Allaah kinga kutokamana na Shaytwaan, akaupuuza na akanyamaza. Huu ndio wasiwasi. 
Ama shaka ni kufuru na ina maana ya mtu kuwa na kusita kati ya mambo mawili; hajui kama ni hivo au sivyo; hajui kama aliyokuja nayo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni sahihi au sio sahihi.

No comments:

Post a Comment