Wednesday, May 11, 2016

JE, 'UMAR (Radhiya Allaahu ´anh) ALISHEREHEKEA NISFU SHA'BAAN?

Swali:
Kuna mapote ambayo yanasherehekea usiku wa Nisfu Sha´baan na wanasema kuwa ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) alikuwa akisherehekea usiku huu. 
Tunaomba utubainishie hukumu?


Jibu Wanamsemea uongo ´Umar. 
´Umar hakuwa anafanya hivi. ´Umar ni miongoni mwa watu waliokuwa msitari wa mbele kabisa kujitenga mbali na Bid´ah na kutahadharisha nazo. 
Usiku wa Nisfu Sha´baan hakukuthibiti kitu na tarehe 15 Sha´baan hakuna swawm. 
Hili halikuthibiti
Hii ni miongoni mwa Bid´ah ambazo Allaah hakuteremsha dalili yoyote juu yake.
Mwenye kutaka kufanya ´ibaadah ashikamane na mambo yaliyowekwa katika Shari´ah na yale yaliyowekwa na Allaah na Mtume Wake.
 Haya yatamtosheleza na Bid´ah.


Mzungumzaji: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Chanzo: Duruus-ul-Haram http://www.alfawzan.af.org.sa/node/14005

No comments:

Post a Comment