Tuesday, May 7, 2019

ADABU ZA RAMADHANI
Kula Sahuwr (Daku)  

Imependekezwa kula sahuwr (daku) na hakuna madhambi kwa yule ambae hakufanya hivyo. Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema: “Kuleni daku, kwani ndani yake kuna baraka” [Al-Bukhaariy na Muslim].

Sababu ni kuwa kula daku kunampa nguvu mwenye Swawm, kunamfanya awe mkakamavu, na kuifanya Swawm kuwa ni nyepesi kwake.

Thursday, September 6, 2018

JE, INAFAA KUTUNZA NGUO ZA MAITI ?

INAFAA KUTUNZA NGUO ZA MAITI ??  

Shaykh Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)



SWALI:

Je, inajuzu kuhifadhi nguo za maiti? Na ikiwa haijuzu, basi ni lilo bora kuzifanya?

EPUKA MAMBO HAYA EWE MUISLAM...!

بسم الله الرحمن الرحيم


Muhammad  Bin 'Abdil-Wahhaab Sulaymaan At-Tamiymiy

Jua ya kwamba mambo yanayomtoa Muislamu katika Uislamu ni mambo kumi:

Moja: 
Ni kumshirikisha Allaah Aliyetukuka katika ibada, Anasema Allaah:
“Hakika Allaah Haghufuri kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae.  Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amepotoka upotofu wa mbali.” (An-Nisaa: 116)
Na Anasema Allaah:
“Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni Motoni. Na madhalimu hawatopata mwenye kunusuru yeyote.” (Al-Maaidah: 72)
na miongoni mwa hizo shirki ni kuchinja kwa asiyekuwa Allaah kama anayechinja kwa ajili ya majini au makaburi.