بسم الله الرحمن الرحيم
Muhammad Bin 'Abdil-Wahhaab Sulaymaan At-Tamiymiy
Jua ya kwamba mambo yanayomtoa Muislamu katika Uislamu ni mambo kumi:
Moja:
Ni kumshirikisha Allaah Aliyetukuka katika ibada, Anasema Allaah:
“Hakika Allaah Haghufuri kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae. Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amepotoka upotofu wa mbali.” (An-Nisaa: 116)
Na Anasema Allaah:
“Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni Motoni. Na madhalimu hawatopata mwenye kunusuru yeyote.” (Al-Maaidah: 72)
na miongoni mwa hizo shirki ni kuchinja kwa asiyekuwa Allaah kama anayechinja kwa ajili ya majini au makaburi.